Mr. Iddi Sandaly,
Bachelors in Accounting, MBA, CPA, CGMA
Controller at
Property Management Company
KUSHIRIKIANA NA KINA MAMA NA WATANZANIA WOTE HAPA DMV

Kwa miaka mitatu mfululizo nimekuwa nikishiriki na kushirikiana na kikundi cha kina mama kwenye matembezi hiari ya Kansa. 
Kikundi cha kina mama wa DMV ndani yake kukiwa na watanzania wenzetu walio pitia janga la Kansa wamekuwa mbele kuwaomba na kuwataka watanzania wachangie kwenye utafiti wa Kansa na pia kuwaomba watanzania wote wafanyiwe uchunguzi wa Kansa. 
Na kwa miaka mitatu toka kikundi hichi cha wana DMV kilipoanza nimekuwa nikishirikiano nao kwa kutoa mchango wa kifedha kwenye utafiti wa Kansa na pia kwa kuwa nao kina mama wa hawa kwenye matembezi.
Lengo na Mipango ni kushirikiana na kikundi hiki cha kinamama na kwa mwaka huu nitashirikiana nao na kuandaa na tutajaribu kuwaleta wataaalamu na huduma ya bure ya uchunguzi wa kansa kwa wana DMV kama nilivyoshirikiana na viongozi wenzangu na Nesiwangu kwenye kuleta huduma ya Bure ya Afya hapa DMV. 
Pia tunafanya maandalizi ya mwakani lili tuweze kupata kina baba wengi kujumuika kwenye Matembezi haya ya Kansa,
DMV KWANZA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 25, 2014

    Hawa jamaa wanavyopigana madongo ya macho katika kampeni zo za uchaguzi sio bure, yaani unaona kabisa hapo kuna ULAJI.Wanaomba KULA na wala sio KURA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...