Baadhi ya Watanzania wanaoishi Visiwani Comoro wakiwa katika picha ya pamoja na Bw. Ali Mwadini (wa pili kutoka kushoto), Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania, Comoro ambaye alimwakilisha Mhe. Balozi Chabaka Kilumanga wakati wa  futari ya pamoja iliyoandaliwa na Watanzania hao kwa kushirikiana na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Moroni. 
Jumuiya ya Watanzania waishio Comoro wakipata futari ya pamoja. 

Jamii ya Watanzania wanaoishi Visiwani Comoro wameandaa futari ya pamoja, kwa kushirikiana na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Moroni. Lengo la futari hiyo lilikuwa ni kuwakutanisha Watanzania wanaoishi Comoro, hususan katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili wajumuike pamoja. 
Wakizunguza wakati wa hafla hiyo, Watanzania hao walielezea kufurahishwa na kufarijika kwao kutokana na kitendo cha Serikali ya Tanzania kufungua Ubalozi nchini Comoro. Walieleza pia utayari wao wa kushirikiana na Ubalozi ili kuhamasisha maendeleo yao na ya nchi kwa ujumla.
Akizungumza katika halfa hiyo kwa niaba ya Mhe. Balozi Chabaka Kilumanga, Bw. Ali Mwadini wa Ubalozi wa Tanzania Moroni, aliwashukuru Watanzania hao kwa kupata wazo zuri la kuandaa futari na kuushirikisha Ubalozi.
Aidha, aliwasihi waendelee na umoja huo kwa kusaidiana na kuwa raia wema kwa kutii sheria za nchi wanapoishi. Aliwakumbusha pia kufika Ubalozini na kujisajili kwa wale ambao bado walikuwa hawajafanya hivyo. Vile vile, aliwahimiza kushiriki katika Kongamano la Watanzania Wanaoishi Ughaibuni linalotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 14 na 15 Agosti 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...