Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (kulia), Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay (kushoto) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu (kulia) akiwa na maofisa wa Benki hiyo kabla ya kuanza kwa mkutano.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei kuzungumza na waandishi wa habari kjuhusu Wiki ya Wateja wa Benki ya CRDB.
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu maadhimisho ya wiki ya Wateja wa Benki ya CRDB itakayoanza Oktoba 6-11.
 Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
-----------------------------------------------
WATANZANIA wametakiwa kutumia huduma za kibenki katika kukuza na kujiongezea uchumi wa maisha yao.

Rai hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei katika mkutano wake na waandishi wa habari kuhusu wiki ya wateja wa benki hiyo itakayoanza Oktob 6,hadi 11,mwaka huu.

Alisema wiki hiyo ni maalum kwa ajili ya kusikiliza kero mbalimbali za wateja ikiwemo kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa.

"Azma kubwa ya maazimisho hayo ni kuwasikiliza wateja na kutimiza mahitaji yao kwa wakati ...lengo la CRDB ni kuboresha na kuinua uchumi wa kila mtanzania kupitia mikopo, kutunza na kukuza amana pamoja na kutoa ajira kwa vijana na misaada kwa jamii"alisema Dk. Kimei.
Akifafanua zaidi alisema kwa kutambua umuhimu na mchango mkubwa wa watanzania kwa CRDB, wanatumia wiki hiyo kutoa huduma bora na kusikiliza kero zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...