Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha-Rose Migiro akikagua Jengo la Mahakama ya Mafunzo katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania leo (Ijumaa, oktoba 24, 2014) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu wake Mhe. Angellah Jasmine Kairuki na kulia ni Mkuu wa Taasisi hiyo Jaji Dkt. Gerald Ndika.
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha-Rose Migiro akikagua Jengo la Mahakama ya Mafunzo katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania leo (Ijumaa, oktoba 24, 2014) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu wake Mhe. Angellah Jasmine Kairuki na kulia ni Mkufunzi wa Taasisi hiyo Bw. Goodluck Chuwa.
Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania Jaji Dkt. Gerald Ndika (kulia) akiongea na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha-Rose Migiro nje ya Jengo la Mahakama ya Mafunzo katika Taasisi hiyo leo (Ijumaa, oktoba 24, 2014) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu wake Mhe. Angellah Jasmine Kairuki na kulia ni Mkufunzi wa Taasisi hiyo Bw. Goodluck Chuwa. (Picha na Martha Komba, Wizara ya Katiba na Sheria).

Serikali inakamilisha taratibu za kuwasilisha Bungeni Muswada wa Sheria unaolenga kurekebisha Sheria ya Bodi ya Mikopo ili kuwawezesha wanafunzi wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) kupata mikopo kwa ajili ya mafunzo yao.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Asha-Rose Migiro amewaambia wanafunzi wa taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa, Oktoba 24, 2014) kuwa lengo la Serikali kukamilisha mchakato huo katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia sasa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...