Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw.John Haule (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa tarehe 21 hadi 25 Oktoba, 2014. Wiki hiyo ambayo huadhimishwa kila mwaka itajumuisha gwaride rasmi na kupandishwa bendera katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam tarehe 24 Oktoba. Sherehe hizo zitahitimishwa na bonanza la michezo mbalimbali litakalo husisha wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje kwenye viwanja vya Gymkhana tarehe 25 Oktoba. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni "Agenda ya Maendeleo baada ya 2015 - Asiachwe mtu nyuma (The Post 2015 Development Agenda - leaving No one Behind)". Wakwanza kushoto ni Bwa. Alvaro Rodriguez, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, na wakwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy.
Wawakilishi wa Idara na Vitengo kutoka Mambo ya Nje
Bw. Alvaro Rodriguez akizungumza na waandishi wa Habari
Waandishi wa Habari kutoka mashirika mbalimbali ya habari hapa nchini wakisikiliza maelezo kuhusu maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa.
Picha na Reginald Kisaka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...