Na   Bashir  Yakub

Nimewahi kuandika  mara  kwa  mara  kuhusu  utaratibu  mzuri  wa  kumwezesha  mtu kununua nyumba  huku  akiwa ameepuka  mgogoro. Nilitahadharisha  sana  kuhusu  migogoro  ya  ardhi  ambayo  sasa  imekuwa  janga  la  kitaifa  hapa  kwetu. Nakumbuka  moja  kati  ya  mambo  niliyoeleza   ni  kuwa utaratibu  wa  manunuzi  ya  nyumba/viwanja unatofautiana.Nikasema kwamba  tofauti  zake  zinatokana  na  ukweli  kuwa   kila  nyumba  ina mazingira  yake. Hata  hivyo sikusema  utofauti  wa  mazingira  hayo ila  sasa  naweza  kueleza  kwa ufupi  utofauti  wa  mazingira  ya  kila  nyumba  unapokuwa  katika  taratibu  za ununuzi. 

1.UTOFAUTI  WA KITAALAM  KATIKA  UNUNUZI  NYUMBA.

Usikurupuke   unapohitaji  kununua ardhi.  Unapaswa  kujua  kuwa   nyumba  na  viwanja  zina  taratibu  tofauti unapohitaji  kununua. Ukikurupuka utalipia  gharama  ya kukurupuka  kwako. Kutokana  na  hilo ni muhimu tujue  kuwa kuna  nyumba  inayouzwa  kwa  utaratibu  wa kawaida  wa mmiliki  mwenyewe    kumuuzia  mnunuzi. Hii  mara  nyingi  huwa  haina  shida sana kwakuwa  unahitaji  tu  kujiridhisha  na baadhi  ya  mambo  ya  msingi   kama  kufanya  upekuzi  rasmi  ( official  search) katika  mamlaka  za ardhi n.k.  

Pili kuna  nyumba  inayouzwa  na  wasimamizi  wa  mirathi. Hii  uuzwaji  wake  hauko  sawa  na   ile  inayouzwa  na  mmiliki halisi.  Hawa  ni wasimamizi  wa  mirathi  hivyo  hata  uuzaji  wao  si  uuzaji  kama  wa mmliki  halisi. Utofauti  wao  upo  katika  namna  ya  kuandika  mkataba( sale agreement) na  nyaraka  ambazo  wanapaswa  kukuonesha  wewe  mnunuzi .  Pia  kuna  ununuzi  wa  nyumba  ya  mkopo  ambao  sasa  ndio  mada  ya leo. Ununuzi wa  nyumba  ya  mkopo  nao  si  ununuzi  kama  wa nyumba  ya  kawaida. Haufanani  na  nyumba  ya  kawaida  na haufanani  na wa  nyumba  ya  mirathi. Unazo  tarati  bu zake  tofauti  kabisa  na ununuzi  mwingine.

2.UMUHIMU WA  KUZINGATIA  UTARATIBU  UNAPONUNUA  NYUMBA YA DHAMANA.

Tatizo kubwa  linakuja  kuwa  unaponunua  bila  kuzingatia  utaratibu  pia  uwe  tayari  kupoteza.  Ieleweke  kuwa nyumba  au  ardhi   yoyote ni kitu  ambacho  hudumu  milele. Hivyo  kama  utakosea  utaratibu  hata   kwa  kiwango  kidogo basi  ya kutosha  kuishi  bila  amani  maisha  yako  yote. Kama  si  wewe  watakuwa  watoto  wako  na  kama  si  watoto  wako  watakuwa  wajukuu  wako.  Kati  ya  hawa   kuna mmoja   mgogoro  utamkuta kwa  makosa  uliyoyafanya  wewe. Na ubaya  wa  mgogoro  unapotokea  mahakama  kikubwa  inachokifanya  ni  kuangalia  nani  alikosea  taratibu.  Inaangalia  hilo  kwasababu  yenyewe  inakuwa  haipo   wakati  mnauziana  na hivyo  nyote  haiwajui  na  haijui  kati  yenu  nani  mkweli  na  nani  muongo.

 Kwahiyo kama ni wewe  mnunuzi  uliyekosea taratibu  wakati  wa kununua  basi   hakuna  kingine  ila  kupoteza  bila   kujali  gharama   ulizotumia  katika  manunuzi. Lakini  ikiwa  ulifuata  taratibu   kwa  umakini  kwanza  ni  vigumu kuingia  katika  mgogoro  lakini   hata  bahati  mbaya uingie katika mgogoro  basi  ushindi  utakuwa  ni  wa  kwako. Huu  ndio umuhimu  wa  kuhakikisha  unafuata  taratibu.  Zingatia  maeneo  mawili  kwanza  uandaaji  wa  mkataba  na  pili ukaguzi  na uhakiki  wa  nyaraka. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...