Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli kushoto akizungumza jambo na Mbunge wa Hai ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Mhe Freeman Mbowe wakati Waziri wa Ujenzi alipokagua barabara ya Kwa sadala-Masama-Machame JCT km 16.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli kushoto akimtaka mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe kuchangia shule mojawapo iliyopo Masama kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa pamoja na mabweni.

 Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Mhe Freeman Mbowe katikati akiwa na Diwani wa kata ya Masama Ali Mwanga wakimpigia makofi Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuchangia shilingi milioni tano kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa madarasa na mabweni katika shule ya Sekondari Kokashu iliyopo katika Kata hiyo ya Masama. Mbunge wa Hai, Mhe Freeman Mbowe naye alichangia kiasi cha Shilingi milioni tano.
 

 Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe akiwa pamoja na Waziri wa Ujenzi wakicheza kwa furaha pamoja na wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara uliohusu ujenzi wa barabara ya Kwa sadala-Masama-Machame JCT km 16.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiangalia nyufa ndani ya jengo la Wilaya ya Siha ambalo lilisimamiwa ujenzi wake na Wakala wa Majengo Tanzania TBA. Waziri Magufuli ametangaza kujengwa upya kwa jengo hilo mara baada ya kubaini kasoro mbalimbali na ametoa muda wa wiki mbili kwa Wakala kuhakikisha wanaanza kazi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Chadema wako juu sana aisee, ila sifa nyingi zitawalevya na kua kama cuf

    ReplyDelete
  2. Tanzania ijayo ikiwa Ina kiongozi mkuu anayefanya kazi zake kwa weledi bila itikadi za vyama na woga Kama MHE. MAKUFULI nchi itakuwa mbali Sana. Mungu tusaidie !!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...