Mwakilishi Mkazi Mwandamizi wa JICA nchini aliyemaliza muda wake Bw. Tomonari Shinya (kushoto) na Mwakilishi Mkazi Mwandamizi mpya wa JICA nchini Bw. Takizawa Koichi (kulia) wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (hayupo pichani) wakati wa hafla fupi ya kumuaga  Bw. Tomonari Shinya iliyofanyika Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo .
 Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kushoto) akizungumza na Mwakilishi Mkazi Mwandamizi mpya wa JICA nchini Bw. Takizawa Koichi (kulia) na aliyemaliza muda wake Bw. Tomonari Shinya (wa pili kutoka kulia) katika hafla fupi ya kumuaga Bw. Shinya iliyofanyika Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.Wengine ni Afisa Tawala Msaidizi wa JICA Bw. Nasibu Hamisi (wa tatu kutoka kulia) na Afisa Tawala  wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bi. Mwanamridu Jumaa (wa nne kutoka kulia).
 Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kulia) akisalimiana na Mwakilishi Mkazi Mwandamizi mpya wa JICA nchini Bw. Takizawa Koichi (kushoto) alipoitembelea Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.
 Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kulia) akipeana kadi za mawasiliano na Mwakilishi Mkazi Mwandamizi wa JICA nchini aliyemaliza muda wake Bw. Tomonari Shinya (kushoto) wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo. Katikati ni Mwakilishi Mkazi Mwandamizi mpya wa JICA nchini Bw. Takizawa Koichi akishuhudia.
Kaimu katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kushoto) akimkabidhi zawadi Mwakilishi Mkazi Mwandamizi wa JICA nchini aliyemaliza muda wake Bw. Tomonari Shinya (kulia) katika hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...