Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa akiwasilisha taarifa ya
maandalizi ya sherehe za Nane Nane Kanda ya Kati zitakazo fanyika
sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Kitaifa kuanzia Agosti
Mosi Mkoani Dodoma.
Sherehe za Nane Nane Kanda ya
Kati zitafanyika sanjari na Maonesho na mashindano maalum ya mifugo ya 5
Kitaifa katika uwanja wa Nzuguni Dodoma kuanzia tarehe 01/08
hadi 08/08/2015.
Sherehe za Nane Nane mwaka huu
2015 zinakwenda kwa Kaulimbiu inayosema “Matokeo
Makubwa sasa (BRN)– Tuchague viongozi
bora kwa maendeleo ya Kilimo na Ufugaji” Kaulimbiu hii imekuja wakati
muafaka ambapo Taifa letu la Tanzania linaelekea katika Uchaguzi Mkuu Mwezi
Oktoba na tayari baadhi ya vyama vya siasa vimeshaanza mchakato wa kuendesha
kura za maoni ili kupata wagombea wa nafasi mbalimbali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...