TAREHE 04 – 09 – 2015
UKUMBI WA MIKUTANO WIZARA YA KAZI NA AJIRA
WCF ni Taasisi ya Serikali chini ya Wizara ya Kazi na Ajira iliyoundwa
kwa Mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ya mwaka
2008 ili kushughulikia masuala ya fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika Sekta ya
Umma na Binafsi Tanzania Bara ambao wataumia, kuugua au kufariki dunia wakiwa
katika utekelezaji wa majukumu ya Mwajiri.
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi
(WCF) umeanzishwa kwa Madhumuni makuu yafuatayo;
·
Kutekeleza matakwa ya Sera ya Taifa ya
Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003 katika kukabiliana na majanga mbalimbali
yanayoikumba jamii ikiwamo ajali, magonjwa au vifo vinavyotokana na kazi;
·
Kutekeleza matakwa ya Kifungu cha 5 cha
Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ya Mwaka 2008;
·
Kulipa fidia stahiki pale mfanyakazi
anapoumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi;
·
Kuwasaidia wafanyakazi watakaoumia au kuugua
kutokana na kazi ili waweze kurudi kazini au kushiriki katika shughuli nyingine
zitakazowapatia kipato (ukarabati na ushauri nasaha);
·
Kuweka utaratibu utakaowezesha kuharakisha
malipo ya fidia kwa wafanyakazi au wategemezi wao;
·
Kuweka utaratibu utakaowezesha Mfuko kupokea
michango kutoka kwa waajiri na kufanya malipo;
·
Kukidhi matakwa ya mikataba ya kimataifa
kuhusu fidia kwa wafanyakazi; na
·
Kukuza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa au
vifo katika maeneo ya kazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...