TAREHE 04 – 09 – 2015
 UKUMBI WA MIKUTANO WIZARA YA KAZI NA AJIRA

WCF ni Taasisi ya Serikali  chini ya Wizara ya Kazi na Ajira iliyoundwa kwa Mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ya mwaka 2008 ili kushughulikia masuala ya fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika Sekta ya Umma na Binafsi Tanzania Bara ambao wataumia, kuugua au kufariki dunia wakiwa katika utekelezaji wa majukumu ya Mwajiri.

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umeanzishwa kwa Madhumuni makuu yafuatayo;
·        Kutekeleza matakwa ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003 katika kukabiliana na majanga mbalimbali yanayoikumba jamii ikiwamo ajali, magonjwa au vifo vinavyotokana na kazi;
·        Kutekeleza matakwa ya Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ya Mwaka 2008;
·        Kulipa fidia stahiki pale mfanyakazi anapoumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi;
·        Kuwasaidia wafanyakazi watakaoumia au kuugua kutokana na kazi ili waweze kurudi kazini au kushiriki katika shughuli nyingine zitakazowapatia kipato (ukarabati na ushauri nasaha);
·        Kuweka utaratibu utakaowezesha kuharakisha malipo ya fidia kwa wafanyakazi au wategemezi wao;
·        Kuweka utaratibu utakaowezesha Mfuko kupokea michango kutoka kwa waajiri na kufanya malipo;
·        Kukidhi matakwa ya mikataba ya kimataifa kuhusu fidia kwa wafanyakazi; na 
·        Kukuza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa au vifo  katika maeneo ya kazi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...