Timu
ya Menejimenti ya HakiElimu ikiwa katika picha na Mwenyekiti wa Bodi ya
HakiElimu na Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa jopo la washauri
bingwa.
Wafanyakazi wa Shirika la HakiElimu waliohudhuria uzinduzi katika picha ya pamoja na jopo la washauri bingwa
Waliosimama
ni Prof. J. Galabawa (kushoto) Prof. Kitila Mkumbo (katikati) na Prof.
Elias Jengo (kulia) Waliokaa ni John Kalage (Mkurugenzi wa HakiElimu)
Prof. G.Mmari (katikati) na Prof. Prof. Martha Qorro (Kulia).
Mgeni
rasmi Prof. Geofrey Mmari,akizungumza jambo katika hafla fupi ya
uzinduzi wa jopo la washauri mabingwa akitoa neno la ufunguzi.
Prof. Kitila Mkumbo mmoja wa wajumbe wa ThinkTank akitoa neno kwa niaba ya jopo la washauri bingwa wa HakiElimu.
Mwakilishi
wa Kamishna wa Elimu Bi, Joyce Sekimanga kutoka Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi akiwasilisha ujumbe kutoka serikali katika uzinduzi wa
jopo la washauri wa HakiElimu
Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu John Kalage akielezea lengo la kuanzishwa kwa Think Tank
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
SHIRIKA la HakiElimu
limezindua Jopo la Washauri Mabingwa
linaloundwa na maprofesa 10 waliobobea katika fani ya elimu ili kuleta mabadiliko katika sekta ya elimu kwa
watoto kupata elimu bora.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es
Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu , John Kalage amesema kazi ya jopo
hilo itakuwa kutoa ushauri wa kitaalam juu ya masuala ya elimu kadri
litakavyoombwa na HakiElimu.
Amesema jopo hilo litatoa ushauri juu ya mikakati
,taratibu na mbinu za kuhakikisha ushiriki madhubuti katika kukuza na kutetea
ubora wa elimu nchini.
Kalage aliwataja maprofesa wanaounda jopo hilo kuwa ni
Abel Ishumi,Herme Mosha,Justinian Galabawa,Kitila Mkumbo,Suleiman
Sumra,Martha Qorro, Mwajabu
Possi,Akundaeli Mbise, Masalukulangwa pamoja na Elias Jengo.
Amesema kuanzishwa kwa jopo hilo litasaidia shirika
kupata mawazo mapana zaidi ya kitafiti na uchambuzi wa changamoto za sekta ya
elimu.
Kalage amesema kuwa jopo hilo litakwenda sambamba na
jitihada za serikali kuwa na mikakati mingi ya kuboresha elimu na azma ya
serikali kutekeleza maazimio mbalimbali ya kimataifa kama Malengo Maendeleo Endelevu (SDGs) na Incheon ya
uboreshaji wa elimu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...