Na Bashir Yakub.
1.JE KITU GANI KIFANYKE ASKARI ANAPOKUNYIMA DHAMANA.
Kwanza ieleweke kuwa dhamana ni haki yako. Haki ni jambo la lazima. Haki ya dhamana inaruhusiwa kunyimwa katika makosa machache sana kwa mfano uhaini, wizi wa silaha, mauaji n.k. Makosa mengine madogo madogo hasa haya ya kila siku ya kutukana, kudhalilisha, kupigana, ajali ndogo, wizi usio wa silaha, na mengine dhamana ni lazima. Hata hivyo makosa ambayo hayaruhusiuwi kwa dhamana ni lazima askari anapokunyima dhamana aandike sababu za kukunyima dhamana.
Na hapohapo yatakiwa ahakikishe anakufikisha mahakamani haraka sana iwezekanavyo hasa ndani ya saa 24 ili mahakama ikatizame shauri lako na haki unazostahili. Ni makosa makubwa askari kumnyima raia dhamana pale anapostahili na ni makosa makubwa askari kutomfikisha mtuhumiwa mahakamani haraka bila sababu za msingi. Unayo haki ya kumtaka askari akufikishe mbele ya hakimu/jaji haraka ili ukaombe dhamana huko na haki zako nyingine. Katika hili hautaomba ila utamtaka askari kufanya hivyo.
2. JE DHAMANA NI LAZIMA UWEKE(DEPOSIT) YA KIASI CHA FEDHA.
Hapana dhamana si lazima uache pesa. Unaweza ukapewa dhamana kwa ahadi ya maandishi tu. Ahadi ya maandishi ni masharti ambayo utayasaini na kuahidi kuyatekeleza utapokuwa umeachiwa kwa dhamana. Moja ya masharti hayo ni kuahidi kufika tena kituo cha polisi au mahakamani katika muda utakaopangwa. Dhamana ya kuweka kiasi cha fedha huwa inaamriwa iwapo kuna makosa makubwa yaliyotendeka. Hata hivyo fedha hizo hutakiwa kurudishwa ama baada ya upelelezi kukamilika na kuonekana mtuhumiwa hana kosa au baada ya kuwa huru kutokana na amri ya mahakama.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...