Na  Bashir  Yakub.

1.JE  KITU  GANI  KIFANYKE  ASKARI  ANAPOKUNYIMA  DHAMANA.

Kwanza  ieleweke  kuwa  dhamana  ni  haki  yako. Haki  ni  jambo  la  lazima.  Haki  ya  dhamana  inaruhusiwa  kunyimwa  katika  makosa  machache  sana kwa  mfano  uhaini, wizi  wa  silaha,  mauaji n.k.  Makosa  mengine  madogo madogo hasa  haya  ya kila  siku  ya  kutukana,  kudhalilisha, kupigana,  ajali ndogo, wizi  usio  wa  silaha, na  mengine   dhamana  ni  lazima.  Hata  hivyo  makosa ambayo  hayaruhusiuwi  kwa  dhamana   ni  lazima  askari  anapokunyima  dhamana  aandike  sababu  za  kukunyima  dhamana.  

Na  hapohapo  yatakiwa  ahakikishe  anakufikisha  mahakamani  haraka  sana  iwezekanavyo  hasa  ndani  ya  saa  24  ili  mahakama  ikatizame  shauri  lako   na  haki  unazostahili.  Ni makosa  makubwa  askari  kumnyima  raia  dhamana   pale  anapostahili  na  ni  makosa  makubwa  askari  kutomfikisha  mtuhumiwa  mahakamani  haraka  bila  sababu  za  msingi.  Unayo  haki  ya  kumtaka  askari   akufikishe  mbele  ya  hakimu/jaji   haraka  ili  ukaombe  dhamana  huko na  haki  zako  nyingine.  Katika  hili hautaomba  ila   utamtaka  askari kufanya  hivyo. 

2. JE  DHAMANA  NI  LAZIMA  UWEKE(DEPOSIT) YA KIASI  CHA  FEDHA.

Hapana  dhamana   si  lazima  uache  pesa. Unaweza  ukapewa  dhamana  kwa  ahadi  ya  maandishi  tu.  Ahadi  ya  maandishi   ni  masharti  ambayo  utayasaini   na  kuahidi  kuyatekeleza  utapokuwa  umeachiwa  kwa  dhamana.  Moja  ya  masharti  hayo   ni  kuahidi  kufika  tena  kituo  cha  polisi  au  mahakamani  katika  muda  utakaopangwa.  Dhamana ya  kuweka  kiasi  cha  fedha  huwa inaamriwa   iwapo  kuna  makosa  makubwa  yaliyotendeka.  Hata  hivyo  fedha  hizo  hutakiwa  kurudishwa  ama  baada  ya  upelelezi  kukamilika  na  kuonekana  mtuhumiwa  hana  kosa au  baada  ya  kuwa  huru  kutokana  na  amri  ya  mahakama. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...