Mwalimu Kulthum R. Mussa (Mwambambale) wa Nyakato National
Mwanza anasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Mumewe Dr. Hassan Marekero Mdee (pichani) kilichotokea katika Hospitali ya Bugando Mwanza tarehe 22.11.2015.
Msiba upo
nyumbani kwake Nyakato National Mahina karibu na kanisa la Roma. Heshima za
mwisho zimetolewa siku ya Jumanne nyumbani kwa Marehemu
Mahina. Marehemu atasafirishwa leo Jumatano alifajiri kuelekea Moshi Uchira
kwa mazishi ambayo yatafanyika siku ya Alhamisi.
“Innalilahi Wainnailahi
Rajiun”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...