Na Nizar Visram 

HATIMAYE mazungumzo ya amani kuhusu Syria yaliyokuwa yakifanyika jijini Geneva yamesitishwa bila mafanikio. Msuluhishi kutoka Umoja wa Mataifa (UN), Bw Staffan de Mistura kuanzia tarehe 31 Januari mwaka huu alikutana na pande zinazopigana – upande wa serikali ya Rais Bashar Assad na upande wa waasi kutoka makundi mbalimbali. 

Kulikuwepo na waasi waliounda kile walichokiita kamati kuu ya mazungumzo (High Negotiations Committee - HNC) inayoungwa mkono na Saudia. Kamati hii inaongozwa na Riad Hijab. Wao walimwambia Mistura kuwa hawatashiriki mazungumzo mpaka serikali ya Syria itakapositisha mabomu yake na kuruhusu misaada ifikishwe kwa “raia waliokuwa wamezingirwa na majeshi ya Syria” 

Kikundi cha Wakurdi wa Syria walizuiliwa na Uturuki kwa sababu inawahesabu kama magaidi. Wakurdi hawa wana nia ya baadae kuungana na Wakurdi wenzao walioko Iraq na Uturuki ili kuunda taifa lao la Kurdistan. Hii ndio sababu ya kimsingi kuchukiwa na utawala wa Uturuki

Upande wa serikali uliongozwa na Balozi al-Jaafari ukajibu kwa kusema hilo halina tatizo, kwani pande zote zinapaswa zikubaliane  kama raia wa Syria. Jaafari ni balozi wa Syria huko UN. Yeye alisema Mistura ameshindwa kutoa orodha ya wapinzani watakaoshiriki katika mazungumzo. Hivyo kuna uwezekano mazungumzo haya yakashidikana kama ilivyokuwa wakati wa mazungumzo ya mwaka 2014
Mazungumzo yalichelewa kuanza kutokana na mgawanyiko miongoni mwa wapinzani wa rais Bashar al-Assad.  Bw Mistura alishinikizwa na Marekani pamoja na Saudia, Uturuki na Qatar ambao walilazimisha kuwa HNC peke yao watambuliwe badala ya kuwaachia Wasyria wajiamulie wenyewe. Hii HNC iliundwa na utawala wa Saudia ili kuwakilisha wapinzani wote wa rais Assad

Wakamweka Riad Hijab kama kiongozi wa HNC. Huyu aliwahi kuwa waziri mkuu wa rais Assad. Inasemekana alishawishiwa na nchi za magharibi kujiunga na upinzani, baada ya kupewa sanduku la minoti kutoka majasusi wa Ufaransa

Msemaji mkuu wa HNC ni Mohammed Alloush, ambaye anaongoza kikundi cha Jaysh al-Islam, Hawa ni wafuasi wa madhehebu ya Wahabi ambao wanashirikiana kwa karibu na Al Qaeda kupitia kikundi cha Jabat al-Nusra pamoja na ISIL/Daesh.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...