Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa akikagua ujenzi wa Daraja la Ruvu chini lenye urefu wa mita 140 katika barabara ya Msata –Bagamoyo, Daraja hilo linatarajiwa kukamilika Oktoba mwaka huu.
Mkandarasi wa Estim Construction anayejenga daraja la Ruvu chini akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa alipokagua ujenzi huo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mkandarasi wa Estim Construction kukamilisha ujenzi wa Daraja la Ruvu chini kwa wakati.
Muonekana wa nguzo za Daraja la Ruvu chini lenye urefu wa mita 140 ambalo ujenzi wake unaendelea katika barabara ya Msata-Bagamoyo.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...