Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa akipokea msaada wa bando za bati kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Corporate Bank, Bwana Frank Nyabundege (wa pili kushoto) kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika Mkoa Mpya wa Songwe.Wa kwanza Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashuri ya Mbozi, Erik Ambakisye akifuatiwa na Mbunge jimbo la Vwawa Josephat Hasunga

Benki ya TIB Corporate leo imetoa msaada wa mabati mia moja kwa mkoa wa Songwe ili kusaidia kukabiliana na upungufu wa vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na vyoo mkoani humo.

Mkoa wa Songwe, ambao ni miongoni mwa mikoa mipya, itatumia mabati hayo katika shughulli za ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa wilaya za Mbozi, Mamba, Ileje, Songwe na Tunduma.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Benki ya TIB Corporate, Bwana Frank Nyabundege alisema msaada huo umelenga kuonyesha nia na jitihada za benki yake katika kusaidia kukuza elimu na pia kuunga mkono serikali katika jitihada zake za kuboresha elimu nchini.

'Serikali pekee yake haiwezi kukuza sekta ya elimu hivyo basi ni muhimu tuisaidie serikali katika kuboresha sekta ya elimu kwa kuaanda mazingira mazuri kwa vijana wetu kujisomea’ alisema Nyabundege.

Akitoa shukrani zake kwa benki ya TIB Corporate, Mkuu wa mkoa wa Songwe Mheshimiwa Chiku Gallawa alisema mchango huo ni muhimu katika kukuza na kuboresha sekta ya elimu ambayo ndio kichocheo cha ukuaji wa sekta ya uchumi na kijamii kwa taifa la kesho.

‘Tunaishukuru benki ya TIB Corporate kwa jitihada zake za kushirikiana na serikali katika kukuza sekta ya elimu kwani hakuna taifa linaloweza kuendelea bila kuwa na raia wasomi ' alisema Mheshimiwa Gallawa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...