Na Chalila Kibuda, Globu  Jamii.
IDARA ya Uhamiaji nchini imekutana na Idara ya Uhamiaji ya nchini Zambia kujadili masuala ya uhamiaji kati nchi mbili juu wananchi katika nchi hizo kufuata taratibu za uhamiaji.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Naibu Kamishna wa Idara ya Uhamiaji na Msemaji wa Idara hiyo, Abbas Irovya amesema  kuwa kuna watanzania walikamatwa nchini Zambia 4000 ambao walikuwa wanajishughulisha na ususi.

Irovya amesema kuwa kuna watu wanaghushi hati ya kusafiria na kudai kuwa wanataiboresha ili wasiweze kughushi hati hizo na wataobanika kuwa na hati hizo watachukuliwa hatua katika vyombo dola.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji wa Zambia, Moola Milomo amesema kuwa kuna fursa za ususi nchini humo na kutaka watanzania kufuata utaratibu wa idara ya uhamiaji.

Amesema kuna changamoto kwa watu wanaoingia nchini Zambia lakini Tanzania na inakabiliwa nazo hivyo kunahitaji utatuzi.
  Naibu Kamishna wa Idara Uhamiaji, Abbas Irovya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na maswala mbalimbali yanayojitokeza kwenidara hiyo kati ya Tanzania na Zambia.
Naibu Kamishna wa Idara ya Uhamiaji, Abbas Irovya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji nchini Zambia, Moola Milomo.
Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji nchini Zambia, Moola Milomo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kumaliza mkutano wa kujadili masula ya uhamiaji kati ya nchi Zambia na Tanzania. Kushoto ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abbas Irovya.





Baadhi ya Watendaji mbalimbali Idara ya Uhamiaji wa Tanzania na Zambia wakiwa katika mkutano wa kujadili masuala ya uhamiaji kati ya nchi ya Tanzania na Zambia katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...