Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza na watendaji wa wizara ya Katiba na Sheria jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Harrison Mwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa wizara ya katiba na sheria jijini Dar es Salaam leo.

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Harrison Mwakyembe amesema Serikali inazisubiri Tume ya Uchaguzi nchini (NEC) na Tume ya Uchaguzi Zanziba (ZEC) zimalize majadiliano yao ili mchakato wa kuipigia kura ya maoni Katiba Inayopendekezwa ufanyike.

Mhe. Mwakyembe ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam alipokutana na uongozi wa Kikosi cha Kupambana na Haki za Mirathi  (KIKUHAMI ) kilichoko chini ya Chama cha Wanawake katika Sheria na Maendeleo  Afrika – WiLDAF.

Amesema zoezi hilo lingekuwa limeshakamilika ila Tume za Uchaguzi ziliona ni bora liahirishwe kwanza ili kupisha zoezi la Kikatiba lililokuwa likiikabili nchi la Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana likamilike na kwamba kukamilika kwa zoezi hilo kunatoa fursa kwa Serikali kuendelea na mpango wake wa kuendesha kura ya maoni juu ya Katiba Inayopendekezwa ili kupata Katiba Mpya ya Tanzania.

Aliongeza kuwa Katiba Inayopendekezwa ina vitu vingi sana ambavyo vitasaidia upatikanaji wa haki za wanawake na kuondoa uonevu dhidi yao na hivyo kufanikisha harakati ambazo wadau mbalimbali wa wanawake nchini wamekuwa wakizipigania na hivyo kukamilika wakati Katiba mpya itakapokuwa imepatikana.

Aidha Mhe. Waziri ameutaka uongozi huo wa KIKUHAMI kupitia WiLDAF kuwasilisha Wizarani mapendekezo yao juu ya mabadiliko ya sheria mbalimbali za Mirathi nchini wanazoziona zinawakandamiza wanawake ili ziweze kufanyiwa marekebisho na ziendane na wakati uliopo.

“si mnataka sheria mbalimbali za mirathi zibadilishwe?, leteni mapendekezo yenu , hili ni jukumu letu sote, sisi tupo na hapa wizarani tunao wataalamu watazipitia na kuona namna ya kuzifanyia kazi, ili ziendane na wakati uliopo sasa, alisema na kuongeza kuwa ndio maana amesema Katiba Inayopendekezwa ina vipengele vingi ambavyo vitasaidia kuondoa uonevu kwa wanawake nchini  itakapopitishwa na wananchi kupitia kura ya maoni.”

KIKUHAMI chini ya Uongozi wa Bibi Thabita Siwale ulimuomba Waziiri wa Katiba na Sheria Dkt Mwakyembe kuangalia uwezekano wa kuondoa sheria zinazowakandamiza wanawake hasa zile za mirathi kwani zinawafanya wanawake hasa wajane kunyanyasika katika nchi yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...