Katibu wa Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Binadamu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Separatus Fella, akitoa hotuba ya kufunga Mafunzo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) ya nchini Marekani. Mafunzo hayo yaliratibiwa na Wizara hiyo ambapo yalitolewa kwa Maafisa Wapelelezi wa Jeshi la Polisi, Mahakimu na Waendesha Mashtaka (hawapo pichani) kwa kupewa uelewa na mbinu ya Kupeleleza, Kuendesha na Kusikiliza kesi dhidi ya Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu. Mafunzo hayo ya siku tano yalifanyika katika Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Land Mark, jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Binadamu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Separatus Fella (kushoto), akipokea kitabu kinachoelezea Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu, kutoka kwa Jaji wa Mahakama Kuu nchini Marekani, Virginia Kendall. Taasisi ya Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) ya nchini Marekani, waliandaa mafunzo kwa Maafisa Wapelelezi wa Jeshi la Polisi, Mahakimu na Waendesha Mashtaka kwa lengo la kutoa uelewa na mbinu ya Kupeleleza, Kuendesha na Kusikiliza kesi dhidi ya Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu. Mafunzo hayo ya siku tano yalifanyika katika Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Land Mark, jijini Dar es Salaam.
Jaji wa Mahakama Kuu nchini Marekani, Virginia Kendall, akizungumza na Maafisa Wapelelezi wa Jeshi la Polisi, Mahakimu na Waendesha Mashtaka (hawapo pichani) kabla ya kufungwa mafunzo ya kutoa uelewa na mbinu ya Kupeleleza, Kuendesha na Kusikiliza kesi dhidi ya Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu kwa Maafisa hao. Mafunzo hayo yaliandaliwa na Taasisi ya Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) ya nchini Marekani na kuratibiwa na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Binadamu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Mafunzo hayo ya siku tano yalifanyika katika Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Land Mark, jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Binadamu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Separatus Fella (kulia), Afisa wa Sekretarieti hiyo, Happyness Laizer (wapili kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Taasisi ya Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) ya nchini Marekani, mara baada ya Mafunzo yaliyoandaliwa na Taasisi hiyo yaliyotolewa kwa Maafisa Wapelelezi wa Jeshi la Polisi, Mahakimu na Waendesha Mashtaka kufungwa. Mafunzo hayo yaliratibiwa na Secretarieti hiyo na kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya Land Mark, jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...