NA Estom Sanga- Zanzibar 

Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Balozi Seif Ali Iddi amesema mchango unaotolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kuhamasisha wananchi kupambana na umasikini unapaswa kuungwa mkono kwani unakwenda sambamba na dhamira ya serikali zote mbili za kuwaondolea wananchi kero ya umasikini. 

Balozi Iddi ametoa kauli hiyo alipokutana na baadhi ya wadau wa Maendeleo na Maafisa wa TASAF ofisini kwake mjini Unguja baada ya viongozi na wadau hao wa maendeleo kuhitimisha ziara ya kuwatembelea Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya masikini kisiwani humo. 

Amesema mafanikio makubwa yanayojitokeza katika nyanja za elimu, afya na ongezeko la shughuli za kiuchumi miongoni mwa walengwa wa Mpango huo ni ushahidi tosha kuwa wananchi hususani wale ambao wamekuwa wakikabiliwa na umasikini , wanahitaji kwa kiwango kikubwa utekelezaji wa shughuli za Mpango huo ambao umekuja kwa wakati hasa kutokana na ukubwa wa tatizo la umasikini nchini. 

Balozi Iddi amesema kwa kutambua hilo serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuunga mkono utekelezaji wa shughuli za TASAF kisiwani humo na kuwataka wananchi hususani wale walioko kwenye Mpango wa kunusuru kaya masikini kutumia fursa hiyo vizuri ili hatimaye waweze kuboresha maisha yao. 

Picha ya juu na chini ,Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akizungumza na Wadau wa Maendeleo na viongozi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF ofisini kwake mjini Unguja.
Balozi Seif Ali Idd akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Ladislaus Mwamanga baada ya kupata maelezo ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo kisiwani Zanzibar,anayewaangalia ni Msimamizi wa shughuli za TASAF katika Benki ya Dunia ,Bwana Muderis Mohamed.
Mmoja wa wanafunzi wa shule ya Msingi Kizimbani,Unguja ambaye anatoka kwenye Kaya ya Mlengwa Wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini akikokotoa hesabu, anayemwangalia ni Msimamizi wa shughuli za TASAF katika Benki ya Dunia Bwana Muderis Mohamed.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bwana Ladislaus Mwamanga(aliyesimama)akizungumza na baadhi ya wananfunzi wanaotoka katika Kaya za Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika shule ya msingi Kizimbani kisiwani Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...