Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Alhaj Abdalla Bulembo akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wa Wilaya za Uyui na Tabora mjini, Viongozi wa CCM na watendaji wa Serikali, katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, akiwa katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Tabora, leo.

 Pamoja na kuzungumzia taratibu za uchaguzi ndani ya unaoendelea katika ngazi za mashina, Bulembo amewataka wana CCM, kutambua kuwa sare za CCM zina thamani kubwa kwa kuwa ni za Chama tawala hivyo wazivae hata wanapokuwa wanakwenda kutafuta huduma katika maeneo muhimu, Amewataka pia madiwani kuhakikisha Halmashauri za wilaya zao zinatoa mgawo wa asilimia kumi fedha kutoka mapato yao, kwa ajili ya kuwapatika vijana na kina mama kwa ajili ya mikopo kwa kuwa utaratibu huo upo kisheria.
" Ndugu Bulembo Kazi hii ya Ukuu wa mkoa naipenda sana, hasa kwa sababu nasimamia ilani ya Chama changu, kwa niaba ya Wananchi wa mkoa huu, mpelekee Salaam, Mwenyetiki wetu, Rais Dk Magufuli, kwamba Tabora tunampongeza kwa kazi nzuri anazofanya, mwambie tuna imani naye na tutazidi kumuunga mkono", akisema, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggry Mwanri alipotambulishwa kwenye kikao hicho
Wajumbe wakionyesha bashasha na furaha kwenye kikao hicho
Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggry Mwanri akimtambulisha Mkuu wa Wilaya ya Tabora mjini, Mwalimu Queen Mwanshinga Mlozi, wakati wa mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...