Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, amewataka
makandarasi wazawa wa kampuni ya Samota, Anam na Jossam JV wanaojenga
barabara ya Urambo-Kaliua yenye urefu wa KM 28 kwa kiwango cha lami
wahakikishe wanakamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa muda uliowekwa.
Prof.
Mbarawa ametoa agizo hilo katika kijiji cha Motomoto, Wilaya ya Urambo
mkoani Tabora alipokuwa katika ziara yake ya kikazi ya kukagua mtandao
wa barabara mkoani humo na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa barabara
hiyo.
“Nataka
nione kazi za ujenzi zinafanyika kwa haraka, kwani uzoefu unaonesha
baadhi ya makandarasi wazawa wamekuwa na kasi ndogo, hivyo mjipange
vizuri ili barabara ikamilike kwa wakati”, amesema Prof. Mbarawa.
Amesema
kuwa nia ya Serikali ni kuwajengea makandarasi wazawa uwezo ili waweze
kutekeleza miradi mikubwa mingine ya ujenzi hapa nchini lakini haitasita
kuwanyima kazi hizo kama miradi hiyo itacheleweshwa, haitakidhi viwango
vinavyohitajika na kama hawataonekana eneo la kazi kwa kipindi kirefu.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akizungumza na uongozi wa Wilaya ya Urambo, alipokutana nao katika ziara yake ya kikazi ya kukagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Urambo-Kaliua yenye urefu wa KM 28 inayojengwa kwa kiwango cha lami, mkoani Tabora.
Mbunge wa jimbo la Urambo, Mhe. Magreth Sitta, akimshukuru Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kulia), kwa kufuatilia maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Urambo-Kaliua yenye urefu wa KM 28 inayojengwa kwa kiwago cha lami, mkoani Tabora.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu hatua za mradi wa ujenzi wa barabara ya Urambo-Kaliua yenye urefu wa KM 28 na kusisitiza nia ya Serikali ya kuwajengea uwezo wakandarasi wazawa ili waweze kutekeleza miradi ya ujenzi hapa nchini.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, na uongozi wa wilaya ya Tabora wakipita juu ya daraja la Wala lenye urefu wa mita 34 katika barabara ya Tabora-Pangale yenye urefu wa KM 30, katika ukaguzi wa ujenzi wa barabara hiyo, mkoani humo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...