Meneja Habari, Elimu na Mawasiliano toka Mamlaka ya Elimu
Tanzania Bi Sylvia Lupembe akiongea na waandishi wa habari (Hawapo
pichani) kuhusu jitihada wanazofanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili
kukabiliana na changamoto katika sekta ya elimu,wakati wa mkutano uliofanyika
leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Masoko na Uhusiano
toka benki ya KCB Bi. Christina Manyenye.
Meneja Sheria na Uhusiano toka kampuni ya uuzaji na usambazaji wa
mafuta ya TOTAL Bi. Masha Msuya Akiongea na waandishi wa habari (hawapo
pichani) kuhusu mpango wao wa kutoa zaidi ya madawati 1000 kwa kushirikiana
na wadau wengine , mpango huu utaanza kutekelezwa kwa kuanzia na mkoa wa
Dar es Salaam.kulia ni Mkuu wa kitengo cha Masoko na Uhusiano toka benki ya
KCB Bi. Christina Manyenye.
Afisa Rasilimali Fedha toka taasisi isiyo ya kiserikali ya Social Action
Trust Fund (SATF) Bw. Timotheo Tenga akiwaeleza jambo waandishi wa habari(
hawapo pichani) wakati wa mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni
Meneja Sheria na Uhusiano toka kampuni ya uuzaji na usambazaji wa mafuta ya
TOTAL Bi. Masha Msuya.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo
wakiwasikiliza wawasilishaji toka Mamlaka ya Elimu Tanzania, KCB, TOTAL,
Social Action Trust Fund (SATF) leo Jijini Dar es Salaam.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...