Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
amemteua Ndugu Laurean Rugambwa Bwanakunu (pichani) kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bohari ya
Dawa (MSD).
Taarifa
iliyotolewa Dar es salaam leo, Jumatatu, Julai 6, 2015 na Katibu Mkuu Kiongozi,
Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Ndugu Bwanakunu unaanzia Juni 23,
mwaka huu, 2015.
Kabla
ya uteuzi wake, Ndugu Bwanakunu alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Ariel Glaser
Paediatric AIDS Healthcare Initiative.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
6 Julai,2015
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...