Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye akizungumza na
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Landes
SportBund Niedersachsen e.v ya nchini Ujerumani Bw.Reinhard Rawe kuhusu
jinsi wanavyoweza kushirikiana katika Sekta ya Maendeleo ya Michezo hapa nchini
walipokutana jana Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa
Rais wa Kampuni ya Landes SportBund
Niedersachsen e.v ya nchini
Ujerumani Bw.Reinhard Rawe akimueleza Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa
na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye (kushoto) namna ambavyo kampuni yake inaweza
kushririkiana na Wizara katika Sekta ya Maendeleo ya Michezo hapa nchini
walipokutana jana Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Mhe.Nape Moses Nnauye (katikati) akiangalia zawadi aliyopewa na Ujumbe wa Kampuni ya Landes SportBund Niedersachsen e.v
ya nchini Ujerumani baada ya kumaliza
mazungumzo kuhusu maendeleo ya Sekta ya Michezo
hapa nchini yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Kampuni ya Landes SportBund
Niedersachsen e.v ya nchini Ujerumani
Bibi Angie (wa kwanza kulia) akimueleza jambo Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa
na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye wakati wa mazungumzo baina yao kuhusu
maendeleo ya Sekta ya Michezo hapa nchini yaliyofanyika jana Jijjini Dar es
Salam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Mhe.Nape Moses Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Kampuni ya Landes SportBund Niedersachsen e.v
ya nchini Ujerumani baada ya kumaliza mazungumzo
kuhusu maendeleo ya Sekta ya Michezo
hapa nchini yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...