Maelfu ya waombolezaji leo wamehudhuria mazishi ya aliyekuwa Meya wa jiji la Dar es salaam marehemu Kleist Sykes aliyezikwa leo Alhamisi Novemba 23, 2017 katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Viongozi mbalimbali walihudhuria mazishi hayo ya Marehemu Kleist Sykes, aliyefariki dunia jana Jumatano Novemba 21, 2017, wakiwemo Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jaji Mkuu Mstaafu Mhe. Mohamed Chande Othman na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa aliemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Marehemu Kleist Sykes, ambaye alikuwa mtoto wa marehemu Abdulwahid Sykes, mmoja wa waasisi wa chama cha TANU, na ambaye alipewa jina la babu yake Mzee Kleist Sykes, alikuwa Meya wa jiji la Dar es salaam na pia diwani wa kata ya Kivukoni kati ya mwaka 2000 na 2005. Pia alikuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM
Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Meya wa jiji la Dar es salaam marehemu Kleist Sykes likiwasili katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Novemba 23, 2017
Abraham Sykes, mdogo wa aliyekuwa Meya wa jiji la Dar es salaam marehemu Kleist Sykes akiweka udongo kaburini katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Novemba 23, 2017
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika mazishi ya aliyekuwa Meya wa jiji la Dar es salaam marehemu Kleist Sykes katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Novemba 23, 2017
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa aliemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli akishiriki katika mazishi ya aliyekuwa Meya wa jiji la Dar es salaam marehemu Kleist Sykes katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Novemba 23, 2017
Msanii Dully Sykes akishiriki katika mazishi ya baba yake mkubwa aliyekuwa Meya wa jiji la Dar es salaam marehemu Kleist Sykes katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Novemba 23, 2017
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jaji Mkuu Mstaafu Mhe. Mohamed Chande Othman na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa aliemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Mzee Kingunge Ngombare Mwilu na Mtahiki Meya wa Manispaa wa Kinondoni Mh.Benjamin Sitta wakiwa mazishini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...